07/14/2025
Mjane wa mchezaji wa Ureno, Diogo Jota anaweza kurithi hadi pauni milioni 35 kutoka kwa mali yake kwa usalama wa kifedha wake na watoto wao watatu.
Nyota huyo wa Liverpool, 28, ambaye alifariki dunia pamoja na mdogo yake Andre, 25, katika ajali iliyotokea wiki iliyopita nchini Uhispania, alikuwa amejikusanyia mali wakati wa maisha yake ya soka kwenye Ligi Kuu ya Uingereza.
Miaka miwili ya mishahara hii ilimfanya apate pauni 3,952,000 kabla ya kutimkia Anfield, ambapo miaka miwili ya kwanza ya mkataba wake wa miaka minne wa pauni 83,000 kwa wiki aliweka mfukoni pauni 8,632,000 nyingine.
Kutokana na kipaji chake cha hali ya juu, Liverpool iliongeza mkataba huo kwa miaka mitano mwaka 2022 na kupandisha mshahara wake hadi pauni 140,000 katika kandarasi ambayo ilimfanya apate pauni 21,840,000 kabla ya kifo chake.
Ina maana mapato ya jumla ya Jota ya takriban pauni milioni 34.4 tangu awasili kwenye Ligi ya Premia yanaweza kurithiwa na Rute na wanao.
Iliripotiwa pia kwamba Jota aliwekeza katika nyumba ya vyumba vitano, katika kitongoji cha juu cha Liverpool kaskazini mwa Blundellsands.
Kando na mapato yake kutokana na soka Jota pia alikuwa na mikataba mizuri na Nike na EA Sports ikiingiza kiasi cha pauni milioni 3.3 kwa mwaka na alianzisha timu yake ya Esports iitwayo Luna Galaxy.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Ureno, Jota pia alikuwa na mkusanyiko wa magari ya kifahari yenye thamani ya zaidi ya Pauni Milioni moja yakiwemo Range Rover Sport, Porsche 911 Turbo S, Ferrari 488, Audi Q7 na Mercedes-Benz G63AMG.
Tovuti, The Richest, katika wasifu wa kina wa thamani ya kifedha ya Jota, ilisema: ‘Aliacha nyuma urithi wa kifedha ambao ni wachezaji wachache wa soka waliopata wakiwa wachanga sana.
‘Biashara yake mahiri ililingana na maono yake ya uwanjani, aliacha nyuma mwongozo wa jinsi wanasoka wanavyoweza kujijengea mali na urithi zaidi ya uwanja.’
Msiba wa Jota ulikuja siku 13 tu baada ya kumuoa Rute, mpenzi wake wa utotoni.