05/02/2018
Vituo viwili vya televisheni vilivyokuwa vimefungiwa na serikali ya Kenya kuhusiana na kurusha matangazo ya kujiapisha kwa kiongozi wa upinzani Raila Odinga vimeanza kurusha tena matangazo, lakini kituo cha tatu kimeendelea kufungiwa. Kituo cha NTV kimetangaza kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa kimerejesha matangazo kwenye chaneli zake za kulipiwa, huku KTN News nayo ikirejesha chaneli zake za bure. Kituo cha Citizen kimeendeelea kutokuwa hewani. Vituo hivyo vitatu vilifungiwa baada ya kujaribu kurusha mubashara, hafla ya kujiapisha kwa kiongozi wa muungano wa upinzani NASA, Raila Odinga siku ya Jumanne, k**a rais wa wananchi.