18/02/2026
Ningependa kuwatakia nyote wakristo kwa waislam mfungo mwema wa Kwaresma na ramdhan hii ni safari ya kiroho iliyojaa toba, sala, kufunga na matendo ya huruma.
Ni wakati wa kujitafakari, kujinyenyekeza mbele za Mungu, kuimarisha imani yetu, na kuonyesha upendo wa kweli kwa jirani zetu.
*Biblia inasema*: yoel 2:13
“Nirudieni kwa mioyo yenu yote, kwa kufunga na kulia na kuomboleza.
lakini k**a haitoshi
📖 Injili ya Mathayo 6:16
“Tena mnapofunga, msiwe k**a wanafiki, wenye nyuso za huzuni; maana huharibu sura zao ili waonekane na watu ya kuwa wanafunga. Amin, nawaambieni, wamekwisha kupata thawabu yao.”
*Qur’ani Tukufu inasema*:
“Enyi mlioamini! Mmefaradhishiwa kufunga k**a walivyofaradhishiwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu.” – (Surat Al-Baqarah 2:183)
“Na mfungapo, basi Mimi niko karibu; naitikia maombi ya mwombaji anaponiomba.” – (Surat Al-Baqarah 2:186)
Mwenyezi Mungu atujalie neema ya toba ya kweli, subira katika kufunga, moyo wa huruma na mshik**ano, na atuongoze katika njia ya haki.
Kwaresma njema na Ramadhani Kareem kwa wote. Mungu awabariki na awajalie amani tele.Inshaalah