03/05/2025
TAARIFA KWA UMMA
Tarehe: 04/05/2025
KAMPUNI YA MILLENNIUM STARS ENTERTAINMENT YASHTUSHWA NA KUTUMIWA KWA MUUNDO WA TUZO YAKE YA “BONGO MUSIC AWARDS” NA EAGMA BILA IDHINI
Millennium Stars Entertainment inapenda kuwataarifu wadau wote wa tasnia ya burudani, wasanii, mashabiki wa muziki, vyombo vya habari, na umma kwa ujumla kuwa tumeshtushwa na kuguswa sana na taarifa na ushahidi wa wazi unaoonesha kuwa tuzo iitwayo East Africa Gospel Music Awards (EAGMA) imetumia muundo na muonekano unaofanana kwa kiwango kikubwa na ule wa tuzo yetu halali na ya kipekee – Bongo Music Awards.
Tuzo ya Bongo Music Awards ni ubunifu wa Millennium Stars Entertainment uliobuniwa kwa dhima ya kuenzi na kuthamini mafanikio ya wasanii wa muziki nchini Tanzania. Muundo wake ni wa kipekee, wenye alama ya utambulisho, hadhi, na ubora unaotambulika ndani na nje ya nchi.
Hatukuwahi kutoa ruhusa wala kushirikiana na EAGMA katika kubuni au kutumia muundo huo. Kitendo hiki si tu kwamba ni kinyume cha maadili ya kitaaluma, bali pia kinaashiria ukiukwaji wa haki za ubunifu na utambulisho wa chapa.
Tunawaomba wadau wote kutambua kuwa:
Bongo Music Awards ni tuzo halali ya Millennium Stars Entertainment pekee na Muundo wake wa Kipekee unaitambulisha kwa Upekee wake Nchini Tanzania kwani haijawahi kutolewa na nuandaaji yeyote wa Tuzo Nchini.
Hatuhusiki kwa namna yoyote na tuzo za EAGMA.
Tunachukua hatua rasmi za Kisheria ikiwa ni pamoja na kuwasilisha malalamiko yetu Rasmi katika Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na Katika vypmbo vingine vya Utoaji haki.
Tunaendelea kusimama imara katika kulinda ubunifu wa ndani ya nchi na kuhimiza ushindani wa haki katika tasnia ya sanaa. Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi kadri mchakato unavyoendelea.
Imetolewa na:
Josias Charles
Mkurugenzi-Millennium Stars Entertainment
04/05/2025
.tanzania