Hadithi za Mtaa

Hadithi za Mtaa Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Hadithi za Mtaa, Party Entertainment Service, Kigamboni, Dar es Salaam.

Here is where you can get many things you need daily including Tv Streaming with many more channels about 10,000+ like Sports and Entertainment channels, News channels, Movies channels etc

MZIGO WA MAHABA – SEHEMU YA PILI📝Ray Shayo☎️0678236344Amani alijikuta akitazama simu yake kwa muda mrefu, akipitia ujumb...
30/03/2025

MZIGO WA MAHABA – SEHEMU YA PILI
📝Ray Shayo
☎️0678236344

Amani alijikuta akitazama simu yake kwa muda mrefu, akipitia ujumbe wa mwisho aliotumiwa na Neema. Ilikuwa ni ujumbe mfupi lakini wenye uzito :

"Amani, kuna jambo nataka kukuambia... lakini siwezi kwa meseji. Naomba tuonane."

Moyo wake ulishtuka kidogo. Neema hakuwa mtu wa maneno mengi, na kila aliposema kuna jambo la muhimu, basi hakika lilikuwa na uzito.

"Labda ni kuhusu Faraji…" alijiwazia. Kwa muda mrefu, Amani alikuwa akihisi kuna kitu hakiko sawa kati ya Neema na Faraji, lakini hakujua ni nini hasa.

Alikata shauri, akampigia Neema. Simu iliita mara mbili kabla haijapokelewa.

"Haloo, Neema…" sauti yake ilikuwa ya upole.
"Haloo Amani, umeiona meseji yangu?" Neema aliuliza kwa sauti ya wasiwasi.
"Ndio, na ndio maana nakupigia. Tunaweza kuonana lini?"
"Kesho jioni, sehemu ile ile."

Amani alijua sehemu anayomaanisha – duka la kahawa walilopenda kukutana, mahali ambapo mara nyingi walikaa na kuzungumza kuhusu maisha yao.

Usiku huo, Amani alijikuta akihangaika kitandani. Fikra zake zikiwa na maswali lukuki.

"Neema anataka kuniambia nini?
Labda ni kuhusu Faraji? Au kuna jambo jingine kubwa zaidi?" Amani aliwaza pasipo kuwa na jibu

Kesho yake jioni, alipofika kwenye duka la kahawa, alimkuta Neema akiwa tayari ameketi kwenye kona ya dirisha, akizungusha kijiko kwenye kikombe chake cha kahawa huku akionekana mwenye mawazo mazito.

Amani alipoketi, Neema alimtazama kwa macho yaliyojaa hisia…

"Amani, kuna jambo lazima nikwambie, lakini naogopa litabadilisha kila kitu kati yetu…"

Je, 🤷Neema ana siri gani? Sehemu ya tatu itafichua mambo mazito! Usikose

Mzigo wa Mahaba – Sehemu ya Kwanza📝Ray Shayo☎️0678236344"Bro, huyu demu nitamchukua tu, hata iweje!" Mshikaji wangu Gody...
19/03/2025

Mzigo wa Mahaba – Sehemu ya Kwanza
📝Ray Shayo
☎️0678236344

"Bro, huyu demu nitamchukua tu, hata iweje!" Mshikaji wangu Gody alinitazama kwa macho ya mshangao huku akitingisha kichwa.
"Kwani unadhani mapenzi ni k**a kudai deni la mtaa?" aliuliza huku akijisogeza karibu.

Jina langu ni Brian, lakini mtaa unanijua k**a Brayo. Mchizi wa maisha, kijana wa ghetto, lakini mwenye ndoto za kuwa na maisha mazuri. Nilikuwa nimepanga hesabu kali juu ya Nisha, demu ambaye kila jamaa mtaani alitamani kuwa naye, lakini mimi nilijua huyu ni mzigo wangu wa mahaba.

Tatizo ni kwamba, Nisha hakuwa lelemama.

Mrembo, mwenye pozi, na akili ya mjini.

Hana time na wanaume wa maisha ya kubahatisha.

Anapenda mpango ulio safi—mshiko, heshima, na future yenye uhakika.

Lakini nani k**a mimi? Nilijua kabisa niko mbali na level zake, lakini roho haikukubali kushindwa.

Siku moja, nilimkuta Nisha kwenye duka la Mangi akihangaika kuchagua juice.
Nikajisogeza taratibu, nikaanza game yangu ya akili.
"Unajua... siyo kila juice inafaa kwa mrembo k**a wewe," nilisema kwa sauti ya confidence.

Alicheka kidogo, akaniangalia juu chini, "Sasa unataka kusema mimi nafaa kunywa juice gani?"
Nikajichekesha, "Mimi naona juice ya apple, maana unapendeza k**a tufaha."

Akatabasamu, lakini kabla hajasema kitu, jamaa mmoja akatokezea ghafla!
Alikuwa amevaa suti safi, perfume yake ilishaanza kuniweka kwa wakati mgumu, na Nisha alivyotabasamu alipomuona, nikajua hapa kuna kazi!

Huyu jamaa ni nani? Na je, Brayo ataweza kweli kumchukua Nisha?

Usikose sehemu zijazo katika Mzigo wa Mahaba

Address

Kigamboni
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi za Mtaa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share